Home         Mafunzo Kuhusu Migogoro

       

 

 
 
Online Training
 

Back

  English Version
 
 
 
Country Profiles
Tanzania Tanzania
Kenya Kenya
Burundi Burundi
Rwanda Rwanda
Congo, DR DRC
 
Related Sites
  Peace Clubs
  GNRC
  Inter Kids
 
                                    

 Katika ukurasa huu utaona MIGOGORO, ASILI NAAINA YAKE, na NJIA ZA KUITATUA


Lengo kuu la mada

Lengo kuu la mada hii ni kuwawezesha wadau katika maswala ya Amani,kutafakari juu ya utambuzi,mitizamona na tabia inayohusiana na   migogoro katiak jamii

 

Utangulizi

Migogoro katika jamii ni jambo la kawaida kwa sababu ni sehemu ya maisha ya binadamu .migogoro hutokea kwa sababu kila mtu kwa ubinafsi wake ni tofauti na mwenzake, hivyo kila mtu ana vitu anavyovithamini , ana mahitaji binafsi na shauku binafsi .

 

1.1: MAANA YA MIGOGORO

migogoro maana yake ni vurugu au makabiliano ya silaha ya ana kwa ana au mapambano baina ya vikundi au kikundi, au baina ya dola na dola au madola .katika makabiliano au mapambano hayo watu wanaohusika hujeruhiwa na wengine huuawa

 

Neno migogoro hutumika vilevile kumahanisha vita ya kiraiya, ugomvi WA kiraiya {civil strife,uhasama vita,na udhaifu wa kisiasa{political instability}

 

1.2:CHANZO/ASILI YA  MIGOGORO

Chanzo cha migogoro hutofautiana kutokana na sehemu na sehemu na aina ya migogoro husika . Hata hivyo asili hasa ya migogoro ni tofauti zinazotokana na ubinafsi, mahitaji na shauku za kila binadamu.

 

1.3:AINA YA MIGOGORO

    . Migogoro ya mipaka

    .Vita vya kiraiya na migogoro ya ndani yenye kuleta athari kimataifa

    .Migogoro inayotokana  na urithi  wa madaraka {succession}

    .Migogoro ya kisiasa na kiitikadi

    .Migogoro inayotokana  na ufugaji wa kuhamahama

 

vile vile  kuna migogoro ya kisiasa na vurugu za mjini na vijijini

 

Migogoro ya kisiasa ni kama  :vita baina ya nchi na nchi,vikund vya waasi ya dola {serikali}, mapinduzi ya kijeshi na vikundi vinavyojitenga na waasi

 

Vurugu au migogoro ya mijini {Arban  violence}Hizi zinaweza  kuchukuwa sura ya migogoro ya kikabila, dini au tabaka {masikini wakivamia mali za serikali,au maduka na nyumba za matajiri na wakulima }

 

Migogoro ya vijijini  {Rural Conflict }Hii huwa ni Migogoro ya kikabila hasa kati ya wafugaji na wakulima.

 

     .Tofauti kati ya migogoro ya kisiasa na migogoro ya mjini na vijijini ni kwamba migogoro ya kisiasa dola uhusika kwa namna moja au nyingine migogoro ya mjini na vjijini dola linaweza lisiwe na  wakati mwingine  matukio hayalipotiwi.

 

 

     .Mijgogoro kati ya nchi na nchi: Hii mara nyingi  ilitokana   na mipaka ya kikoloni

 

 

Migogoro ya ndani

Hii ni ya aina nyingi:

       .Ile ambayo dola ni sehemu ya migogoro, hii  uchochewa na siasa

       .Migogoro baina ya vikundi ambavyo dola ni sehemu yake mfano,uasi  dhidi ya serikali iliyoko madarakani, uasi wa kujitenga {secessionist rebellion}

       . mapinduzi ya kijeshi

       .Migogoro iliyotokana na vita baridi

       .Migogoro ya vina yotokana na vikundi vingi kuwa na huchu wa kuongoza nchi.

       . migogoro ya vijijini  kuhusiana na rasilimali.

       .vurugu na migogoro ya mjini.

        

1.4: SABABU ZA KUWEPO MIGOGORO

A. Siasa  

            .Kugombania madaraka ya kuongoza dola

            .Uongozi usio na mwono {vision}  na ushawishi toka nje

            .Kutokuwa na uwazi pamoja na uongozi mmbaya

            .Uvunjaji wa haki za binadamu

b. Uchumi :

            . umasikini

            .ugawaji mbovu wa rasilimali na pato la la taifa

            .Athari za mzingo wa deni lanje na mfumo mbaya wa fedha kimataifa

 

C. Kijamii na Kitamaduni

           . Tofauti za kitabaka katika jamii   

           . Mfumo unaoendekeza utengano katika jamii na huasama wa kikabila

           . Wajibu wanasiasa katika kusikiliza hisia za kikabila na kikanda

           .Tofauti za kitamaduni na kiutafuta utambulisho

           . Mfumo mbaya wa Elimu.

 

1.5:HATUA ZA MIGOGORO

1.5.1:migogoro kabla ya ukoloni

         Migogoro mingi iliusu vita kati ya himaya moja na nyingine, uasi wa ndani dhidi ya watawala, kuzuiya biashara ya watumwa,migogoro   baina ya makabila juu ya malisho,mifugo, ardhi,mauaji ya kulipiza kisasi n.k.

 

 

   1.5.2:Migogoro wakati wa ukoroni

             Mchakato wa kuiivamia Afrika ulisababisha jamii za kiafrika kupinga.Hivyo  waafrika waliingia vitani kutegemea maendeleo ya sehemu husika hata pale  waafrika waliposhindwa na kuwa  chini ya himaya  ya wakoloni migogoro iliendelea kutokana na mabadiliko yaliyo letwa  na wakoloni kama kumiliki ardhi kwa watu binafsi, kodi,shelia mpya n.k.Hivi vyote vilipingwa na vilisbbisha migogoro.      

 

 

1.5.3:Migogoro wakati wa uhuru {1960-2000}

Hii imegawanyika sehemu tatu:

Kipindi cha serikali za kizalendo

 

Kipindi  cha vita baridi  {1970-1989}

Hiki kilikuwa ni kipindi ambacho nchi nyingi za Afrika uchumi wa ke ulidumaa.

Mashirika makubwa ya Fedha duniani  WB naIMFyalianza kutunga sera za kiuchumi

Kwa nchi zilizo kuwa zinaendelea. Sera hizo zilizibana sana nchi za dunia ya tatu na kusababisha kuongezeka kwa  tabaka  kati ya wenye nacho na wasiokuwa nacho.

 

Migogoro baada ya vita baridi {1990-2000}:Baada ya vita baridi mabadiliko mengi yametokea,na ambayo yamesababisha migogoro kuongezeka:

.Wajibu wa WB na IMF na masharti ya kisiasa kati ya wakopeshaji na wakopaji wameongezeka.

.Jumuia za kijamii ndani na nje ya nchi zinazoangalia rekodi za utawala bora na haki za binadamu katika nchi zimeongezeka

.Athari za SAP katika kuongeza umaskini mijini na vijijini na kuongezeka kwa idadi ya watu kumeleta mvutano na migogoro ya rasilimari(ardhi ya kulima/maji n.k)

.Upatikanaji wa siraha ndogondogo kutoka kwa wauzaji wa kimataifa na vikundi vya waasi umeongezeka.

.Utandawazi na biashara ya kimataifa/mikopo yenye masharti magumu,utegemezi wa wawekezaji wa nje na uchumi usio shindani kwa nchi nyingi za kiafrika vimeongezeka.

.Misaada kwa serikali zilizokuwa za kidikteta(ya kifedha na siraha)vimeondolewa.

.2.0;NJIA ZA KUONGOZA NA KUTATUA MIGOGORO(Conflict management  and resolution)

Njia zifuatazo zaweza kutumika pale penye migogoro ili kukabiliana nayo na kuitatua.

.Kuwa na baraza la usuluishi;Hili linatakiwa kuundwa na watu wenye busara kutoka pande mbalimbali za nchi na kanda  mbalimbali za wananchi.

.Mpatanishi kutoka nje ya nchi.

.Kuwa na mfumo bora wa utoaji haki.

.Kuwa na mawasiliano mazuri.

3.0;JINSI YA KUBADILI MIGOGORO(Tranforming conflicts)

Ili kubadili sura ya mgogoro,Pande husika yabidi ifanye mambo yafuatayo;

.Pande zinazohusika kuwa na maandalizi ya kutosha ya b inafsi.

.Pande zinazo husika kuwa na makubaliano ya kukutana (Zikubaliane mchakato wa kumaliza mgogoro,kukaa katika meza ya maeleano,kukubali kuheshimiana,kusiwepo kulaumiana wala kunyanyuliana vidole,kuwepo na uwazi)

.Pande husika zielezee shauku na malengo yao ya mwanzo(mfano uzoefu wao jinsi mgogoro ulivyowaathiri)

.Pande zinazo husika zizidi kuelezea tena shauku na malengo yao(chukua muda wa kutafakari yaliosemwa na mwenzako,ukichukua vitu vya msingi)

.Mkubaliane katika baadhi ya maelezo.

.Endeleeni kuleta shauku zenu,nafasi na hisia na anzeni kutafuta ufumbuzi(katika hili ni muhimu kuwa wawazi,kuainisha vitu vya msingi,mbinu,maeneo mnayokubaliana na msiyokubaliana,jitahidi katika vitu halisi vinavyoweza kupimika).

.Fanyeni majumuisho ya makubaliano na mtoe suluhisho.

.Fatilia (follow up)kuangalia kama suluhisho la mgogoro linatekelezwa na uangalie tena kama unaona inafaa.

4.0;UZUIAJI WA MIGOGORO(Prevention of conflicts).

Ili kuzuia migogoro yatubidi;

1:Kujenga taifa(National buiding):Watu wanatakiwa wajenge na kuendeleza taifa kwa kuwa na sera za kiutamaduni zitakazotekelezwa na mfumo wa elimu.

11:Mfumo wa siasa(Political system):Kuna umuhimu wa kujenga mfumo wa siasa unaruhusu ushindani katika kugombea kupata madaraka ambayo inaruhusu vikundi vingine kupata madaraka katika muda muafaka.Mfumo uwaruhusu watu na vikundi vingine kushiriki katika kuchagua/uchaguzi wa kumpata mtu au watu ambao wanashiriki katika utoaji wa maamuzi katika ngazi mbalimbali za madaraka.Vilevile mfumo wa siasa ni lazima uzingatie mambo haya:

.Kukabidhi ,madaraka kwa wengine kwa amani.

.Kujilimbikizia mali kwa kutumia taasisi za serikali au dola kusiruhusiwe maadili ya utawala bora na demokrasia uzingatiwe(Kuwepo na uwazi,uwajibikaji,mfumo huru wa haki na sheria,na jeshi liwe la wananchi).

.Vikundi vya kijamii vihusishwe katika kuangalia utekelezaji wa sera na utoaji wa huduma.

111:Ukuaji wa uchumi(Economic development):Rasilimari za taifa zigawanywe sawa kati ya kanda na vikundi katika nchi.

1.5:MBINU ZA MAWASILIANO ZINAWEZA KUSAIDIA KATIKA KUBADILISHA MIOGORO.

            .Uwazi

     .Uvumilivu .  

.kuheshimiana.

.Uwezo wa kuhisi maono ya wengine(empathy).

.Maelewano.

 

 
                 
     

GYOPEN| Copyright © 2005 - All Rights Reserved